Kocha George
Lwandamina mwenye umri wa miaka 53 alizaliwa mwaka 1963 Mufulira nchini Zambia
akisimama kama mmoja wa magwiji wa soka nchini humo na Afrika kwa ujumla
kutokana na historia yake nzuri toka akiwa mchezaji na baadae kocha.
Lwandamina
akiwa kama mchezaji aliweza kuimudu vyema nafasi ya mlinzi wa kati. Alianza
kusikika katika soka baada ya mwaka 1984 kujiunga na timu ya Mutondo Stars na
akisimama kama beki wa kati wa kutumainiwa hali iliyomfanya kuitwa timu ya
taifa ya Zambia .
Alidumu na timu hiyo kwa msimu mmoja tu kabla ya kutimkia
timu ya Mufulira ikiwa timu ya nyumbani kwao na hii ni baada ya ushawishi
mkubwa wa viongozi wa timu hiyo.
Alidumu na
Mufulira mpaka january 17, 1989 alipoamua kuachana na timu hiyo. alianza
mafunzo ya ukocha huku akichezea timu mbalimbali lakini si ngazi ya ushindani .
Baada ya kumaliza mafunzo yake 1997 alirudi Mufulira kama kocha mkuu. Hii ni
Mufulira wanderers tofauti na ile Mufulira blackpool , Timu pinzani katika mkoa
wa Mufulira.
Aliachana na
Mufulira mwaka 2000 baada ya kuwawezesha kuwa mabingwa wa ligi kuu na kutimkia
Green Buffaloes aliyoifundisa toka mwaka 2002 hadi mwaka 2009 lakini hakuwahi
kuipa kombe lolote zaidi ya kucheza fainali ya Chibuku mwaka 2005 na kushindwa.
2009 mpaka
2010 alijiunga na Kabwe Warriors timu ambayo aliiwezesha kuwa moto wa kuotea
mbali nchini Zambia na hawa ndio waliomfanya gwiji huyu kupendekezwa na mkongwe
Kalusha Bwalya kuinoa timu ya taifa ya Zambia al maarufu kama Chipolopolo (
risasi za shaba ).
2011 hadi
2014 alijiunga na Red Arrows akiipa ubingwa wa kombe la Barclays mwaka 2013 na
mwaka 2014-15 kuchaguliwa kocha bora nchini Zambia .
Mafanikio na Red Arrows
yaliwafanya mabosi wa Zesco United kumnyakua mwaka 2014 na kuwawezesha kuwa
mabingwa wa ligi 2014 na 2015 mara mbili mfululizo katika ligi yao maarufu sana
kwa jina la ZAMBIAN SUPER LEAGUE ikiwa ligi ya pili kwa ubora kusini mwa Afrika
baada ya ligi kuu nchini Afrika Kusini.
Mwaka huohuo
wa 2014pia aliwawezesha Zesco United kunyakua kombe la Barclays .
Hii ilimfanya
kumpa heshima kubwa nchini humo kwa msimu wa kwanza kuchukua kombe la ligi kuu
na kombe hili la Barclays .
Huyo ndio
George Lwandamina kocha mkuu wa timu ya taifa ya Zambia pia bado ana kandarasi
ya miaka miwili na Zesco United inayoisha February 17 2017.
Mabosi wa Yanga
SC wamemleta nchini kuchukua nafasi ya Hans Van Pluijm na tayari amelamba
kandarasi ya miaka miwili.
|
No comments:
Post a Comment