Bayport Na Miaka 10 ya kutoa Huduma ya Mikopo Nafuu ya kifedha Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, October 26, 2016

Bayport Na Miaka 10 ya kutoa Huduma ya Mikopo Nafuu ya kifedha Tanzania.

Taasisi inayoongoza Tanzania kwa kubobea katika kutoa mikopo nafuu, Bayport Financial Services katika kipindi cha miaka 10  iliyopita  imechangia kwa kiwango kikubwa  katika kuboresha maisha ya maelfu ya Watanzania kupitia  utoaji wa mikopo.

 Bayport Tanzania ni miongoni mwa taasisi tanzu kumi za Taasisi ya Bayport Group ambayo hutoa ufumbuzi wa kifedha  kwa watu binafsi walioko katika ajira rasmi au waliojiajiri ndani ya soko linaloibukia. 

Huduma zinazotolewa na taasisi hiyo  zinaboresha ujumuishwaji kifedha  kwa watu ambao hawana uwezo wa kuzifikia  huduma za kawaida za kibenki  au walio na kiasi kidogo cha fedha katika benki. 

Baada ya kuanza shughuli zake  nchini Zambia mwaka 2001, shughuli za Bayport  kwa hivi sasa zinaendeshwa katika nchi saba barani Afrika na  nchi mbili ndani ya Amerika Kusini. 

Nchi hizo ni Zambia, Uganda, Ghana, Tanzania, Botswana, Afrika Kusini, Msumbiji, Colombia, na Mexico.

 Hivi sasa Bayport  imekuwa ni msingi wa kuaminiwa na mteja ikiwa na  takribani wateja 518,000 ambao  kila mara wamekuwa wakipata  na hata na kufurahia huduma inazozitoa.  

 Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bayport Tanzania, John Mbaga, Bayport imeshatoa  zaidi ya  shilingi bilioni 48 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2015 peke yake. 

Kwa upande mwingine Bayport inachukuliwa kuwa ni ‘mlipa kodi mkubwa’  nchini Tanzania  ikiwa  imelipa  zaidi ya shilingi bilioni 7 kwa mwaka wa fedha 2014.

Matamanio yetu ni  kuboresha maisha ya  wateja wetu  na kuwapa fursa  ambazo zitawanufaisha  sio wao peke yao bali pia  watoto wao na kizazi kijacho,” alisema Mbaga  katika mazungumzo yake na wanandishi wa habari hivi karibuni. 

Aliongeza, “Tunawasaidia kwa kuangalia unafuu utakaotokana na  mtiririko wa fedha katika kipindi kifupi ambapo matokeo yake  husaidia familia katika kuongeza na kuwa na ustawi wa kifedha  wa kudumu.

 Bayport Tanzania  ilianzishwa mwaka 2006, na kwa haraka  imekuwa ni  mtoaji wa mikopo kwa wafanyakazi katika sekta za umma na binafsi. Kuwepo kwa ofisi zake 83 za kudumu na matawi 45 ya muda  kumeifanya  kufika kila mkoa kwa Tanzania Bara.

 Kampuni hii ina wafanyakazi wa kudumu 300 na mtandao wa mawakala wa mauzo zaidi ya 1000. 



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad