Aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa
Kagera, Amantius Msole.
Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli
ametengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Bw.Amantius Msole na
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, Bw.Steven Makonda baada ya
kubaini kuwa wamefungua akaunti nyingine ya benki kwa kutumia jina linalofanana
na akaunti rasmi ya kuchangia maafa iitwayo "Kamati Maafa Kagera" kwa
lengo la kujipatia fedha.
Kwa mujibu wa Ikulu jijini Dar es
Salaam ,taarifa iliyotolewa leo September 27,2016 na Waziri Mkuu, Bw.Kassim
Majaliwa muda mfupi baada ya kupokea hundi ya msaada kutoka kwa Waziri Mkuu wa
India, Mhe.Narendra Modi iimeeleza kuwa pamoja na kutengua uteuzi huo Rais
Magufuli ameagiza vyombo vya dola vichukue hatua dhidi ya wote waliohusika
katika njama za kufungua akaunti hiyo.
Msaada huo ni wa shilingi Milioni 545.
Aidha, Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa
amemsimamisha kazi Mhasibu Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Simbaufoo Swai kutokana na
kuhusika katika njama hizo.
Hata hivyo Waziri Mkuu ametoa wito
kwa wananchi na taasisi mbalimbali kuendelea kuchangia misaada kwa ajili ya
walioathirika kwa kutumia akaunti rasmi ya "Kamati Maafa Kagera"
ambayo imetangazwa na Serikali.
|
No comments:
Post a Comment