|
Safari ya Kilimanjaro Queens kuusaka
ubingwa wa CECAFA Women’s Championship 2016,ilianza Septemba 9 ikiongozwa na
kocha mkuu wa timu hiyo Sebastian Nkoma walikabidhiwa bendera ya taifa na Mkuu
wa Mkoa wa Kagera tayari kuelekea Jinja nchini Uganda baada ya kuhitimisha
kambi ya siku chache mjini Bukoba.
Kabla ya kuelekea Jinja, Kilimanjaro
ilicheza mchezo mmoja wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Burundi na kufanikiwa
kupata ushindi wa magoli 3-0.
Wanadada hao wa Tanzania bara
waliwasili Uganda wakiwa tayari kukipiga kwenye michuano hiyo ya pili kwa
ukubwa kwa wanawake katika ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Tanzania
iliangukia kwenye Kundi B kundi lililokuwa na timu tatu (Tanzania, Rwanda na
Ethiopia).
Ilianza kwa ushindi wa magoli 3-2
dhidi ya Rwanda kisha ikatoka suluhu na Ethiopia na kufanikiwa kufuzu hatua ya
nusu fainali kwa matokeo ya kurushwa shilingi kufuatia kulingana pointi na
Ethiopia.
|
Kwenye husu fainali wakakutana na
wenyeji wa mashindano hayo timu ya Uganga ambapo Kilimanjaro ikafuzu hatua ya
fainali kwa kuichapa Uganda kabla ya kuishinda Kenya na kutangazwa mabingwa wa
CECAFA ya wanawake.
|
No comments:
Post a Comment