Muonekano kwa mbali wa Barabara kuu
inayounganisha Nchi ya Burundi na wilaya ya -Ngara mkoani Kagera - ambayo imekuwa ni msaada mkubwa sana kwa
Wananchi wa nchi za Tanzania,Rwanda na Burundi kuitumia katika shughuli za usafirishaji.
Watu wanaodhaniwa kuwa Majambazi
wamevamia kijiji cha Mabawe wilayani Ngara mkoani Kagera na kumuua mkazi wa
kijiji hicho kisha kupora Mali dukani kwake na kukimbia wakielekea nchini
Burundi.
Mtendaji wa kijiji hicho Bw Joseph
Festo amemtaja aliyeuawa kuwa ni Joseph Maganga mwenye umri wa miaka 24 na
kwamba majambazi hao walimtaka kijana huyo awape fedha na wakati wa mabishano
walimpiga risasi na kufariki papo hapo ambapo Mwili wake umehifadhiwa kwenye Kituo
cha afya cha Mabawe
Amesema katika tukio hilo lililotokea Jana July 27,2016,majira ya Usiku, Mwanafunzi
Nice Mathias anayesoma Darasa la 7 katika Shule ya msingi Mabawe amejeruhiwa
mguuni kwa kupigwa risasi na majambazi hao wakati wakibishana na mwenye duka
baada ya kwenda kushuhudia ubishi huo
Mkuu wa Jeshi la polisi wilayani
Ngara Bw Abel Maige amethibitisha tukio hilo na kwamba mtu mmoja anashikiliwa
na Polisi kwa tuhuma za kuwasafirisha wahalifu kwa pikipiki kuelekea mpakani
mwa nchi jirani ya Burundi.HABARI NA RADIO KWIZERA FM.
|
Thursday, July 28, 2016
Home
HABARI
UHALIFU NGARA:-* Watu wanaodhaniwa kuwa Majambazi wavamia kijiji cha Mabawe ,Waua kisha kupora Mali Dukani.
UHALIFU NGARA:-* Watu wanaodhaniwa kuwa Majambazi wavamia kijiji cha Mabawe ,Waua kisha kupora Mali Dukani.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment