Klabu ya soka ya Yanga SC imezidi
kuusogelea ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu kuafutia
ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Stand United jioni ya leo,May 03,2016 Uwanja wa
Kambarage, Shinyanga.
Ushindi huo ulitokana na mabao mawili
ya washambuliaji wa kimataifa wa Zimbabwe, Donald Ngoma na Amissi Tambwe wa
Burundi, unaifanya Yanga ifikishe pointi 68 baada ya kucheza mechi 27.
Yanga SC sasa imebakiza pointi nne
pekee ili itangaze ubingwa wa Vodacom Tanzania bara kwa msimu huu wa 2015-2016.
Stand United walipata goli la kwa
mkwaju wa penati uliokwamishwa wavuni na Elius Maguri dakika ya 81 kipindi cha
pili baada ya Thabani Kamusoko kumuangusha mchezaji wa Stand kwenye box.
Bao hilo la Maguri ni la 12 kwenye
ligi msimu huu.
Matokeo hayo yanaifanya Yanga SC
indelee kujichimbia kwenye kilele cha Ligi huku ikihitaji pointi nne tu kutetea
ubingwa wake.
Yanga SC sasa imefikisha pointi 68,
kama itapata pointi nne itafikisha jumla ya pointi 72 ambazo haziwezi kufikiwa
na Azam FC wala Simba SC hata kama zitashinda michezo yao yote minne iliyosalia
ambazo.
Azam FC inapointi 59, ikishinda mechi
zake zote nne itafikisha jumla ya pointi 71, Simba SC pia ina pointi 58 na
ikishinda mechi zake zote zote itafikisha pointi 70 na kuiacha Yanga ikitwaa taji
hilo kwa mara nyingine tena.
Ligi hiyo kuu soka Tanzania bara
itaendelea tena hapo kesho Jumatano Mei 4, 2016 Azam FC ya Dar es Salaam
itakuwa mwenyeji wa JKT Ruvu ya Pwani kwenye Uwanja wa Azam, Chamazi nje kidogo
ya jiji la Dar es Salaam.
|
No comments:
Post a Comment