Mkuu wa Idara ya Siasa,
Mawasiliano ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale (katikati) akisalimiana na Mkuu wa
Mkoa wa Mwanza, John Mongella mara baada ya kuwasili ofisini kwake mwishoni mwa
wiki.
Hospitali ya Bungando yenye uwezo wa
vitanda 950 iliyoanzishwa mwaka 1972 ni miongoni mwa hospitali nne kubwa nchini
ambazo hutoa tiba maalumu ikihudumia watu milioni 16 katika mikoa minane ya
kanda ya ziwa.
Hospitali hii inatoa tiba ya ugonjwa
wa saratani kwa mifumo miwili. Moja kwa kutumia onkolojia au patholojia na tiba
kwa kutumia mionzi.
Toka mwaka 2000 hospitali ya Bugando
imekuwa ikifanyakazi kwa karibu na kampuni ya kitaliano ya TISSON ASSOCIATION
ili kuboresha huduma zake patholiojia na pia kuanza kutibu kansa mwaka 2009.
Wataliano wamewezesha kufundishwa kwa
wataalamu wa patholojia na onkolojia ya tiba, vifaa tiba, dawa na kuwezesha
ziara za za kifundi za watu wa patholojia na utafiti.
Uangalizi wa wagonjwa wa kansa na
matibabu yao ulianza mwaka 2009 na kuelezwa kuwa kwa mwaka wagonjwa 3500 wa
kansa huangaliwa.
Huduma ya uangalizi ni pamoja na
kufanya utambuzi, upasuaji na utoaji wa tiba ya kemo.
|
Mtaalamu wa Mawasiliano
wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akitoa utambulisho wa ujumbe
alioambatana nao kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.
Hata hivyo wagonjwa wanaohitaji
huduma ya mionzi hukatiwa rufaa hospitali ya kansa ya Ocean (ORCI).
Kutokana na kuzidiwa kwa hospitali ya
Ocean Road katika tiba ya mionzi, serikali iliamua kutanua huduma zake na
kuzifikisha Bugando.
Ili kuwezesha haja ya serikali
taasisi ya nguvu za atomiki duniani na ile ya hapa nchini kupitia mpango wa
ushirikiano wa kiufundi walianzisha miradi kadha yenye lengo la kuwezesha
huduma yenye tija kwa wagonjwa wa kansa.
Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambayo yanachangia miradi hiyo imekuwa
ikisaidia serikali ya Tanzania kuwezesha tiba ya mionzi katika hospitali ya
Bugando.
|
Kutoka
kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa
Mwanza CP. Clodwig Mtweve, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa
nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez, Mkuu wa
Mkoa wa Mwanza, John Mongella pamoja na Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano ya
Umoja wa Ulaya, Luana Reale wakiwa wameshilikilia kuhamasisha utekelezaji wa
malengo mapya ya maendeleo endelevu (SDGs) ambayo yamewafikia wakazi wa jiji la
Mwanza.
|
Mkuu wa
Mkoa wa Mwanza, John Mongella akiwa kwenye mazungumzo na Mratibu Mkazi wa
Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo
(UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mkuu wa Idara ya Siasa, Mawasiliano
ya Umoja wa Ulaya, Luana Reale katika ziara maalum ya kukagua miradi mbalimbali
inayofadhiliwa na UN pamoja na EU jijini humo.
|
No comments:
Post a Comment