Bondia Mohamed Matumla, akiwa amebebwa juu na mashabiki wake baada ya
kutangazwa mshindi katika pambano lake la kimataifa la raundi 10 na Bondia Xin
Hua kutoka nchini China lililomalizika usiku wa March 27,2015, kwenye Ukumbi wa Diamond
Jubilee.
Katika pambano hilo Matumla Jr, alionekana kumzidia Mchina huyo
aliyekuwa akilalama muda wote kuwa anachezewa rafu na mpinzania wake.
Na katika mapambano mengine ya utangulizi, Thomas Mashali kwa mara
nyingine tena ameingia mitini kumkacha mpinzani wake Karama Nyilawila, ambaye
ilibidi abadilishiwe bondia na kupigana na Ibrahim Tamba, ambaye pia alimshinda
kwa KO katika raundi ya mwisho ya nane.
Pambano jingine lilikuwa ni kati ya Japhet Kaseba, aliyepigwa kwa KO na
Mada Maugo katika raundi ya saba kati ya nane zilizokuwa zimepangwa kuchezwa,
huku pia Ashraf Suleiman, naye akimchapa mpinzani wake Bernard Adie, kutoka
nchini Kenya kwa KO katika raundi ya tatu, ambapo Bondia kutoka Mrekani
aliyekuwa acheze na Ashraf, imeelezwa kuwa hakuweza kufika kutokana na sababu
kadha wa kadha zilizomkwamisha.
Na katika pambano la raundi nane lililokuwa la kuwania ubingwa kwa
mabondia wanawake kati ya Bena Kaloki kutoka Kenya na Asha Ngedele,
lilimalizika kwa Mkenya kutwaa ubingwa huo kwa kumchapa Mtanzania kwa KO katika
raundi ya nne.
Pata
Picha, Habari za Kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na Michezo kila stori inayonifikia wakati wowote ukijiunga na mimi kwa kubonyeza…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
No comments:
Post a Comment