Mabasi ya kwenda mikoani yakiwa yamepaki baada ya
wananchi kufunga barabara.
Kwa mujibu
wa shuhuda wa tukio hilo, tukio hilo limetokea leo asubuhi kufuatia mwanamke
ambaye hakufahamika jina lake kujigonga ukutani na kuanguka kisha kufariki
dunia wakati akiwakimbia Polisi waliokuwa kwenye oparesheni ya kuwakamata watu
wanaokunywa pombe wakati wa asubuhi.
Habari zaidi
zinapasha kwamba, licha ya kuchoma moto magari, waliziba barabara kuu ya kwenda
mikoani na kuyazuia magari kupita, hali iliyosababisha Polisi kuwakabili
lakini walizidiwa nguvu na kuingia ndani ya basi la Nyagawa.
Askari
wakiwa ndani ya gari hilo waliendelea kushambuliwa na wananchi kwa mawe na
kuvunja vioo vyake na habari zinasema wananchi kadhaa wamejeruhiwa katika
kadhia hiyo.
|
No comments:
Post a Comment