UPDATES ZA MATOKEO YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA 2014:-Wilaya ya Ngara,Kibondo,Ukerewe,Manispaa ya Bukoba na Singida. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, December 16, 2014

UPDATES ZA MATOKEO YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA 2014:-Wilaya ya Ngara,Kibondo,Ukerewe,Manispaa ya Bukoba na Singida.

Ndugu ‘Kipara’ baada ya kutangazwa mwenyekiti mpya wa mtaa Katatolwanso Kashai-Bukoba.Picha na:-Harakati News.

Hapo chini ni baadhi ya matukio katika picha wakati wa kutangazwa matokeo katika mtaa wa KATATOLWANSO ambapo Ukawa wameshinda huku,vingozi wa Chadema wakiongozwa na Wilfred Lwakatare wakiwa nyuma ya msimamizi wa uchaguzi Bi Hapynes Grayson.

Matokeo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Desemba 14,2014 nchini kote, yanaonyesha kuimarika kwa upinzani nchini baada ya kupata viti vingi vya uenyekiti wa mitaa na vijiji, pamoja na mamia ya wajumbe wa Serikali husika.

Katika Manispaa ya Bukoba yenye mitaa 66 iliyokuwa na ushindani mkali kati ya wagombea wa CCM na wenzao kutoka UKAWA, matokeo ni kwamba  CCM imeshinda mitaa 35 huku UKAWA wakipata mitaa 31.

Kwa Bukoba Mjini kulitakiwa kupatikana wajumbe  330  na kati yake UKAWA wameshinda wajumbe 205 huku  CCM  wakipata wajumbe 125.

Wilayani Karagwe yenye mitaa/vijiji 18 CCM imeshinda vijiji/mitaa 6 tu huku UKAWA wakishinda Vijiji/Mitaa 12.


NGARA.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera Bw Cornel Ngudungi amebatilisha matokeo ya uchaguzi katika vitongoji vya Mnyange na Mukasasa kwenye kijiji cha Murukulazo na kuagiza uchaguzi urudiwe kesho baada ya kujitokeza dosari kadhaa ikiwemo idadi ya kura kuzidi ile ya waliopiga kura

Bw Ngudugi ambaye ndiye Msimamizi Mkuu wa uchaguzi huo amesema hayo leo kufuatia wagombea wa Chadema na CCM kugoma kusaini fomu ya matokeo baada ya kubaini kuongezeka kwa idadi ya kura tofauti na idadi ya wapiga kura waliojiandisha katika kituo hicho

Amesema kitendo cha kuongezeka kwa idadi ya kura tofauti na idadi ya walioandikishwa ni kosa kubwa hivyo uchaguzi unapaswa urudiwe baada ya kushauriana na viongozi wa vyama vya siasa na kamati ya ulinzi na usalama

Diwani wa kata ya Murukulazo Bw Mkiza Byamungu amesema kura 9 zimeongezeka katika kituo cha Mukasasa na kwamba katika kitongoji cha Mnyange walikoshinda CCM ambapo baadhi ya wapiga kura wamezuiwa kupiga kura baada ya majina yao kuwekewa alama kuwa tayari wamepiga kura


KIBONDO.

Chama cha Mapinduzi, CCM Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma kimeongoza katika uchaguzi wa Serikali za mitaa kwa kupata viti 34 vya Wenyeviti wa vijiji kati ya nafasi 50 zilizoshindaniwa sawa na asilimia 76

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo msimamizi Mkuu wa uchaguzi Wilayani Kibondo Bw Judethadius Mboya amesema Chadema wamepata viti 9 sawa na asilimia 12, NCCR Mageuzi viti vitano sawa na asilimia 9 huku Chama cha Wananchi CUF kikipata viti viwili sawa na asilimia 1.4

Amesema katika nafasi ya vitongoji CCM imepata viti 284, Chadema viti 47, NCCR Mageuzi wamepata viti 33 huku Chama cha Wananchi CUF kikipata viti vitano

Bw Mboya amesema wilaya ya Kibondo imefanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuchagua Wenyeviti wa vijiji 50, Wenyeviti wa vitongoji 369 na wajumbe wa serikali za vijiji 700

MWANZA.

Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe Mkoani Mwanza imekamilisha zoezi la kuchambua matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa kwa ngazi ya vijiji, ambapo Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeongoza

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo Bw Octavian Mapunda amesema Chadema kimeshinda katika vijiji 47 kati ya vijiji 76

Amesema Chama cha Mapinduzi CCM kimeshinda kwenye vijiji 27 huku Chama cha Wananchi CUF kikishinda kwenye kijiji kimoja pekee

Amesema zoezi la kuchambua matokeo ya ngazi ya vitongoji bado linaendelea ambapo amewaomba wananchi kuwa watulivu ili kutoa muda wa kutosha kukamilisha kazi hiyo

Bw Mapunda amesema wilaya hiyo ina jumla ya vitongoji 512 ambapo kati ya hivyo vitongoji vinne havikufanya uchaguzi na kwamba vitarudia uchaguzi huo.


SINGIDA.

Chama cha Mapinduzi katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida kimepata ushindi wa wastani wa asilimia 95 katika uchaguzi wa serikali za Mitaa

Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Bw Joseph Mchina ambaye ndiye Msimamizi wa Uchaguzi katika eneo hilo amesema zoezi la upigaji kura, kuhesabu hadi kutangaza matokeo limefanyika kwa amani na utulivu

Akitangaza matokeo hayo Bw Mchina amesema kati ya Mitaa 50 iliyopo katika Manispaa hiyo, Chama cha Mapinduzi kimepata ushindi wa asilimia mia moja baada ya kushinda viti vyote na kuwabwaga wapinzani wake wa CUF, Chadema na ACT

Bw Mchina amesema kati ya vijiji 20 vilivyopo, CCM imeshinda vijiji 19 sawa na asilimia 95 wakati chama cha wananchi CUF kimepata kiti kimoja kwa nafasi ya Uenyekiti

Kwa upande wa vitongoji, CCM imepata ushindi wa asilimia 90, CUF asilimia 8.9 wakati Chadema kimeshinda kwa asilimia 1.1

Chanzo:-Radio Kwizera FM-Ngara/Harakati News.
UNGANANASI KATIKA  FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad