![]() |
|
Mtoto wa
kiume anayekadiriwa kuwa na umri wa siku moja ameokolewa na wasamaria wema toka
kwenye shimo la choo akiwa bado hai bada ya mama yake mzazi kumeza dawa
kwa lengo la kutoa mimba na kumtupa ndani ya shimo hilo.
ITV imefika
katika kituo ch afya cha PK kilichopo kibaoni tegeta manisipaa ya
kinondoni jiji la Dar-es-salaam na kukutana na harakati za wahudumu wa
afya wakijaribu kunasua mabaki ya kinyesi kwenye mwili wa kiumbe huo,aliyetupwa
kwenye shimo la choo katika eneo la tegeta machakani.
Wakiongea na
ITV baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo akiwemo mama aliyekuwa na muhifadhi kwa
muda binti anayedaiwa kutupa kichanga hicho wamesema kuwa watoto walipata
taarifa ya mlio wa sauti wa mtoto ukisikika toka kwenye choo cha shimo kabla ya
kuchukua hatua za kuvunja choo hicho na kutoa mwili wa kiumbe huyo.
Bi Aisha
Mohamedi anayedaiwa kutupa kichanga hicho kwenye shimo la choo amesema
kuwa,awali mzazi mwenzake alimlazimisha kutoa mimba hiyo bila mafanikio na hata
kudiriki kumtishia kwa silaha aina ya kisu,na ndipo alipozidiwa na kupewa
vidonge na mzazi mwenzake kwa minajili ya kutoa ujauzito huo na kukiri kujutia kosa
lake hilo.
Mganga
mfawidhi katika kituo cha afya cha PK Dkt Mashaka Mwanula amethibitisha
kupokea mtoto huyo wa kiume aliyeokolewa baada ya kutupwa ndani ya choo
na hivyo kumpatia huduma ya kwanza kwa kumsafisha huku wakitarajia kumpeleka
katika hosipitali ya wilya ya kinondoni mwananyamala kwa uchunguzi zaidi wa
afya ya mtoto huyo.
Juhudi za kumpata kamnada wa polisi mkoa wa kipolisi
kinondoni ACP Camilius Wambura kuthibitisha tukio hilo zinaendelea.
Habari Na:-ITV.
UNGANANASI
KATIKA FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Tuesday, December 16, 2014
Home
HABARI
MAAJABU YA BINADAMU:-Mtoto mwenye umri wa siku moja aokolewa ndani ya shimo la choo baada ya mama yake mzazi kumtumpa,Tegeta.
MAAJABU YA BINADAMU:-Mtoto mwenye umri wa siku moja aokolewa ndani ya shimo la choo baada ya mama yake mzazi kumtumpa,Tegeta.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.






No comments:
Post a Comment