Waziri Pinda
ametiwa hatiani na kamati hiyo kutokana na kujua kuwapo kwa ufisadi huo na
kauli zake kuwa fedha hizo hazikuwa mali ya umma, wakati Mwanasheria Mkuu Jaji
Frederick Werema ameonekana kutoishauri vizuri Serikali na pia kuagiza fedha
hizo zitolewe kwenye akaunti hiyo, wakati Waziri Sospeter Muhongo hakuchukua
hatua wakati akijua kuwapo kwa sakata hilo, huku naibu wake, Stephen Masele
akitiwa hatiani kwa kulidanganya Bunge.
Kamati pia
imependekeza uteuzi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakimu
Maswi utenguliwe kutokana na kuingia makubaliano ya kutoa fedha bila ya
kujiridhisha kikamilifu kuhusu uamuzi wa hukumu ya mahakama ya Kituo cha
Kimataifa cha Utatuzi wa Migogoro ya Kiuwekezaji (ICSID).
Iwapo
mjadala huo, unaotazamiwa kuendelea leo November 27, 2014, utaafiki hatua hizo
zichukuliwe, Rais atalazimika kuunda Serikali upya kwa mara ya pili tangu
alipofanya hivyo mwaka 2008 wakati wa sakata la Richmond, ambalo lilihusu
umeme.
Pia atakuwa
akifanya mabadiliko ya mawaziri kwa mara ya tano kutokana na wasaidizi hao
kujikuta kwenye kashfa.
“…Katika
fedha ambazo zimelipwa kwa watu binafsi katika Benki hizi yapo majina ya
viongoozi wa kisiasa, viongozi wa madhehebu ya dini, Majaji na watumishi
wengine wa Serikali..“– Zitto Kabwe.
Kwa upande
wa Viongozi wa Kisiasa walioingiziwa fedha katika akaunti zao binafsi ni;
-
Mheshimiwa Andrew Chenge Mbunge, ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na
sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, shilingi Bil.
1.6.
Mheshimiwa Anna Tibaijuka Mbunge na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya
Makazi, shilingi Bil. 1.6.
Mheshimiwa William Ngeleja Mbunge na ambaye alikuwa
Waziri wa Nishati na Madini, shilingi milioni 40.4.
Ndugu Daniel Yona ambaye
alikuwa pia Waziri wa Nishati na Madini shilingi milioni 40.4.
Ndugu Paul
Kimiti, ambaye ni Mbunge mstaafu wa Jimbo la Sumbawanga shilingi milioni 40.4
na ndugu Enos Bukuku ambaye alikuwa Mjumbe wa Bodi ya TANESCo aliingiziwa
shilingi milioni 161.7…“– Zitto Kabwe.
|
No comments:
Post a Comment